Sunday, November 18, 2012

HOTUBA YA DR SHEIN KIBANDA MAITI JANA

NA HAMED MAZROUY
Makamu mwenyekiti wa chama cha mapinduzi zanzibar ambae pia ni rais wa zanzibar na mwenyekiti wa baraza la mapinduzi zanzibar dr ali mohd shein amevitaka vyama vya siasa nchini kut
Oingiliana katika kutekeleza sera za vyama ili kuepusha migogoro kwa wananchi.
Dr shein ameyasema hayo katika mkutano uliofanyika katika uwanja wa demokrasia kibanda maiti mkutano ambao ulipata bahati ya kuhudhuriwa na viongozi mbali mbali wa ccm kama vile balozi seif ali idi na mke wake mama asha na miongoni mwa viongozi wengine ni bi asha rise migiro pamoja na shamsi vua nahoza wakati alipokuwa akizungumza na wanachama na wapenzi wa ccm katika mkutano uliofuatia sherehe za mapokezi yalionza 16-11 akitokea dodoma baada ya kupata ushindi wa aina yake katika kuchaguliwa kuwa makamo mwenyekiti wa ccm kwa upande wa zanzibar ambapo kabla ya hapo nafasi hiyo ilikua inashikiliwa na rais mstaafu wa awamu ya sita ya serikali ya mapinduzi ya zanzibar dr amani abeid karume,
Dr shein amefahamisha kuwa serikali ya umoja wa kitaifa {suk} sio jambo geni bali ni urithi kutoka kwa marehemu abeid amani karume ambae alikua mstari wa mbele katika kusisitiza amani, upendo, utulivu na kuondoa ubaguzi pamoja na chuki za wenyewe kwa wenyewe hivyo chama cha ccm kinaunga mkono suk kama ilivyowezwa kuunga mkono na dr kiketwe katika mkutano mkuu wa nne uliofanyika dodoma..
Akizungumzia suala la uvunjifu wa amani zanzibar dr shein amesema ikiwa yeye kama ni rais wa zanzibar anawaperemba tu wale wanaofanya fujo, hivyo amelisifu jeshi la polisi kwa kazi kubwa walioifanya ya kurudisha amani nchini hivyo amesema serikali itaendelea kuimarisha ulinzi amani na utulivu na wala haitomvumilia yeyote yule atakaesababisha uvunjifu wa amani nchini hivyo amewaomba wananchi kuacha kutumia vivuli vya dini kusababisha fujo nchini kwani suk inatoa uhuru wa kuabudu na sio kuleta uharibifu,,
Aidha dr shein amesema kuwa wao kama chama cha ccm wataendelea kushinda kupitia sera zao zisizo na ubaguzi wala uchafuzi wa amani yoyote na kuahidi kuwa chama hicho kitafanya vizuri katika chaguzi zote zijazo sambamba na hayo dr shein aliendelea kusema kuwa wao kama chama wanafahamu kama kuna muungano wa serikali mbili tu na daima hautovunjika wala wao muungano wa mkataba hawaujui kabisa hivo basi wanaosema kuhusu muungano wa mkataba sijui n

0 comments:

Post a Comment

 
Design by M.S Chopoti | Bloggerized by Ulimwengu Wa Digital