Tuesday, November 27, 2012

Rais Zuma awachinjia Ng'ombe wahenga


Bwana Zuma, ambaye ana wake zaidi ya mmoja na watoto 21, anasifika sana kama mwenye kufuata itikadi za utamaduni wa Zulu.
Rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma amewataka wazee wa jadi au wahenga kumsaidia katika kushikilia uongozi wa chama tawala (ANC).

Bwana Zuma alihudhuria sherehe moja kijijini siku ya Jumapili, ambako ng'ombe 12 walichinjwa na huku ubani ukichomwa watu wakimuombea achaguliwe tena.
Wapinzani wake wanataka ang'olewe kutoka katika uongozi wa chama, huku kongamano la chama likitarajiwa kufanyika mwezi ujao.
Bwana Zuma, ambaye ana wake zaidi ya mmoja na watoto 21, anasifika sana kama mwenye kufuata itikadi za utamaduni wa Zulu.

0 comments:

Post a Comment

 
Design by M.S Chopoti | Bloggerized by Ulimwengu Wa Digital