Friday, November 23, 2012

Vietnam na Zanzibar zakubaliana kuimarisha uhusiano


Na Rajab Mkasaba
 
Hanoi,Vietnam 23.11.2012
ZANZIBAR na Vietnam zimekubaliana kuimarisha uhusiano na ushirikiano katika kukuza sekta za maendeleo na uchumi huku Vietnam ikiahidi kuiunga mkono Zanzibar katika kuhakikisha inafikia malengo yake iliyojiwekea katika kuimarisha sekta za maendeleo na uchumi .
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Ali Mohamed Shein alisema kuwa ipo haja ya kuimarisha na kukuza uhusiano na ushirikiano wa kihistoria uliopo kati ya Tanzaniaikiwemo Zanzibar na Vietnam hasa katika sekta za maendeleo na uchumi.
Dk. Shein aliyasema hayo leo wakati alipokuwa na mazungumzo na Makamu wa Rais wa Vietman Mhe. Bi Nguyen Thi Doan huko katika ukumbi wa Ikulu ya nchi hiyo mjini Hanoi.

Ziara ya Dk Shein Vietnam - siku ya pili

  Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed shein, akisalimiana na Makamo wa Rais Vietnam Bibi, Nguyen Thi Doan,alipowasili Ikulu nchini Vietnam,akiwa na ujumbe wake katika ziara rasmi ya Kiserikali nchini humo ya wiki moja
 Mke wa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mama Mwamamwema Shein, akisalimiana na Makamo wa Rais wa Vietnam Bibi, Nguyen Thi Doan,alipowasili Ikulu nchini Vietnam,alipofuatana na Rais wa Zanzibar katika ziara Rasmi ya Kiserikali Nchini Vietnam ya wiki moja

0 comments:

Post a Comment

 
Design by M.S Chopoti | Bloggerized by Ulimwengu Wa Digital